Thursday 3 March 2011

Mapishi ya Half cake (Keki)


Mahitaji
Unga wa ngano (self risen flour) kikombe 1na 1/2
Sukari (sugar) 1/4 kikombe
Barking powder 1/2 kijiko cha chai
Magadi soda (bicarbonate soda) 1 kijiko cha chai
Mafuta 2 vijiko vya chai
Mafuta ya kukaangia
Maji ya uvuguvugu kiasi

Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.

3 comments:

  1. Asante sana kwa hili

    ReplyDelete
  2. asanteni sana na m-barikiwe. maana leo nimefanya kitu cha tofauti nyumbani kwangu

    ReplyDelete
  3. asante kwa recipes zako mama ntilie vipi kwenye half cake huweki amila na ukiwe itakuwaje? please nijulishe

    ReplyDelete